Mshikamano Wajumbe,
Baada ya viongozi wa THTU kutoa tamko lao kuhusu mgogoro wa ISW kwenye vyombo vya habari ndipo Waziri wa Afya alivyowaita viongozi wa THTU na kufanya nao kikao tarehe 29/09/2011 na ifuatayo ni attachment ya THTU kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.
KIKAO CHA THTU NA MHE. WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII
KILICHOFANYIKA TAREHE 29/09/2011 DSM.
Chama cha THTU kimejihusisha na mgogoro wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii
kikamilifu na kimefanya utafiti wa kina na kubaini kwamba matatizo ya Taasisi
ya Ustawi wa Jamii yanaweza kumalizika na Taasisi kupatiwa ithibati na kurejea
katika hali ya kawaida iwapo yafuatayo yatafanyika kwa haraka:-
(i) Kuwarudisha wafanyakazi wote 30 waliofukuzwa kazi bila masharti
yoyote.
(ii) Kuwaondoa Viongozi wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii ambao hawana sifa
kwa mujibu wa NACTE na ambao ndiyo chanzo cha matatizo, na
kuweka viongozi wenye sifa ili Taasisi irejee katika hali yake ya kawaida.
(iii) Kurekebisha Bodi ya Magavana ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii kwa kuwa
haikidhi matakwa ya Bodi ya Taasisi ya Elimu ya Juu ikiwa ni pamoja na
kutokuwa na wawakilishi wa Wanataaluma, chama cha Wafanyakazi na
Baraza la Wafanyakazi.
(iv) Mhe. Waziri atengue maamuzi yaliyofanywa yakubadilisha mwakilishi wa
NACTE katika Bodi ya Magavana.
(v) Mhe. Waziri atuhakikishie kwamba Wizara na Bodi ya Magavana
wataheshimu maagizo ya NACTE na kuhakikisha kwamba yanatekelezwa.
(vi) Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii itambue kwamba Taasisi ya Ustawi wa
Jamii ni Taasisi ya Elimu ya Juu na si Idara mojawapo ya Wizara na Wizara
iisimamie Taasisi kwa kupitia Bodi ya Magavana.
(vii)Mhe. Waziri atuhakikishie kwamba Wizara, Bodi ya Magavana na
Menejimenti hawaingilii shughuli za vyama vya wafanyakazi.
NIA NA MWELEKEO WETU DAIMA NI KUJENGA!
“TAIFA KWANZA”
THTU stands for The Tanzania Higher Learning Institutions Trade Union. It is an organisation registered on the 12th December 2008 (Reg. No. 23) under the Tanzania Trade Union Registration Act. THTU was established primarily to provide a national forum for Higher Learning Institutions' workers to deliberate on matters that affect workers welfare, Institutional welfare, productivity and broader community interests that impinge on their ability to participate effectivelly in national development.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Tumekiomba chama, nguvu hizi sasa wazielekeze na hapa UDOM. Tunataka uharakishwaji wa kesi zinazotukabili.
ReplyDeleteKwa juhudi tunazofanya sasa, tunaamini tutafika! Insha Allah